KLH News PodcastWhere Tanzania is the news!
Karibu wiki moja iliyopita Mhe. Zitto Kabwe alizungumza na jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la Michigan nchini Marekani. Mazungumzo hayo yaliyofanyika wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyoandaliwa Bw. Zitto yaligusia mambo mbalimbali na hasa kuwataarifu wanajumuiya hiyo mambo mbalimbali yanayoendelea nyumbani na pia kusikiliza maoni na maswali yao.
Matangazo ya leo basi ni hotuba ya Mhe. Zitto kwa jumuiya hiyo na sehemu ya maswali na majibu, yote ni uncut and an edited. Makosa mengine yoyote ya kurekodi hasa mwanzoni kidogo ni ya KLHN.
Pichani Mhe. ZItto akijiandaa kuzungumza na wanajumuiya ya TAMI - Tanzanians Association of Michigan. Huko Detroit eneo la Maili Nane.
Pichani baadhi ya wananchi wakijaribu kuvuka mto. Kidaraja hicho sasa hakipitiki tena. Picha kwa hisani ya Mjengwa
Mvua za masika zimezidi kupamba moto nchini na zimekuwa zikisababisha mafuriko sehemu mbalimbali. Baadhi ya maeneo ambayo yamepata mafuriko ni pamoja na Vunjo, Same na Kyela. Hata hivyo hadi hivi sasa ni wilaya ya Kyela ambayo ina kata 15 ambazo kati ya hizo 11 zimepatwa na mafuriko makubwa .
Siku ya Jumamosi nimepata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Jimbo la Kyela Dr. Harrison Mwakyembe (CCM) kuhusu athari za mafuriko hayo na mahitaji ya msaada. Kwa kifupi hali ilivyo ni kuwa:
a. Kaya 9000 hazina mahali pa kuishi, zimekosa chakula, au athari ya moja kwa moja iliyotokana na mafukio hayo
b. Hadi hivi sasa watu wawili wamefariki
c. Madhara makubwa katika mashamba ya mpunga kiasi kwamba kuna uwezekano kuwa kwa mara ya kwanza Kyela itahemea chakula mwaka huu.
d. Mvua kubwa namna hii hazijawahi kunyesha Kyela kwa karibu miaka thelathini sasa.
e. Juhudi za kuleta misaada zinaendelea ambapo JWTZ imepeleka kikosi chake cha Uhandisi, huku Msalaba Mwekundu wakiandaa misaada ya vitu mbalimbali.
Dr. Mwakyembe anaomba msaada wa Watanzania wote popote pale walipo kuweza kusaidia wananchi wenzao ambao ni kama wamepatwa na "Kimbunga cha Katrina" kwani wengi sasa wanaishi makanisani na kwenye mashule na afya zao ziko hatarini hasa kutokana na uwezekano mkubwa wa kuibuka mlipuko wa magonjwa yanayoambukizwa kwa maji kama typhoid, kuhara damu, salmonella, na pia ongezeko la Mbu wasababishao Malaria.
Kwa yeyote aliyeko Dar, unaweza kutuma mchango wako kupitia:
Kyela Development Fund MNB Bank House Acct No: 2013300198
Au Wasiliana na Dr. Mwakyembe kupitia simu Namba: 255 754 284130
kwa maelekeo ya kuweza kutoa mchango wako kupitia yeye mwenyeweTafadhali sikiliza mahojiano yangu na Dr. Mwakyembe. KLH News imeahidi kutoa msaada wa Shilingi laki mbili kama sehemu ya jitihada za kuwasaidia wananchi wa Kyela
Mwanzoni sikuyaelewa maneno ya Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere kuwa “Bila CCM Madhubuti nchi yetu itayumba”. Nilifirikia kuwa alimaanisha “Bila CCM” nchi yetu itayumba, na pia nilidhania alimaanisha kuwa “Bila viongozi wa CCM” nchi yetu itayumba. Miaka hii ilivyopita na hasa baada ya matukio yaliyolikumba Taifa letu ndio maana hasa ya maneno yake imeanza kuniingia na kwa hakika nimekubali kuwa bila Chama cha Mapinduzi ambacho ni “madhubuti” basi Taifa letu liko matatani, na kwa hakika litayumba.
Kabla hujaanza kunirarua nisikilize hapa au kwenye http://www.klhnews.com